Majukumu ya kisheria

Kwa mamlaka ya sheria ya uanzishaji, [sheria ya wahasibu na wakaguzi (usajili) (sura ya 286 RE: 2002) kama ilivyoelezwa chini ya kifungu cha 4, Bodi ya Taifa ya wahasibu na wakaguzi (NBAA)

Ina mjukumu na mamlaka yafuatayo:

  • Kuendeleza na kutoa fursa na nyenzo za kuchunguza, kufundisha, uhasibu, ukaguzi na masomo shirikishi;
  • Kuendesha mitihani na kutoa diploma, vyeti na tuzo nyingine za Bodi katika uhasibu, ukaguzi na masomo shirikishi.
  • Kudhamini, kupanga na kutoa nyenzo kwa ajili ya mikutano semina na majadiliano, na ushauri kuhusu mambo yanayohusu uhasibu na masomo shirikishi
  • Kupanga kwa ajili ya uchapishaji na usambazaji wa jumla wa machapisho yaliyotokana na shughuli za bodi
  • Kueleza viwango na miongozo ya uhasibu au ukaguzi kadiri inavyofaa na kuhakikisha utimizwaji wa viwango na miongozo kwa masomo husika.
  • Kutunza rejesta ya wakaguzi, wahasibu, watunza vitabu na kampuni/mashirika yanayofanya kazi hizo.
  • Kufikiria na kuamua maombi ya usajili na kufanya usajili wa wakaguzi, wahasibu, watunza vitabu na kampuni/mashirika yanayofanya kazi hizo.
  • Kusimamia shughuli na mwenendo wa wakaguzi, wahasibu, watunza vitabu na kampuni/mashirika yanayofanya kazi hizo.
  • Kutathimini sifa za uhasibu wa nje kwa ajili ya kusamehewa sehemu ya mitihani ya Bodi.
  • Kutunga muundo wa uhasibu wa Taifa na mitaala ya mafunzo na kusimamia mitaala yote ya mafunzo ya uhasibu kwenye taasisi za mafunzo nchini kote inafuata muundo wa uhasibu wa Taifa
  • Kutathimini sifa za uhasibu wa taasisi za ndani kwa ajili ya kusamehewa sehemu ya mitihani ya Bodi
  • Kufanya majukumu mengine baada ya kushauriana na Waziri

Majukumu ya kisheria ya Bodi yaliyotajwa hapo juu yamefupishwa kama ifuatavyo:-

  • Usajili
  • Usimamizi
  • Uendelezaji taaluma ya uhasibu
  • Uwekaji Viwango
  • Kufanya majukumu mengine baada ya kushauriana na Waziri